Kuna watembeleaji 237 wapo online
Pata yanayojiri Tanzania.

Barabara hii sasa itakuwa ya kiwango cha lami. Jana JK aliweka jiwe la msingi pale Migoli.

Waziri wa Nchi ofis ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji) Merry Nagu akiomba kutengua kanuni ya Bunge Na. 38 ili kuruhusu suala la vurugu za Mtwara kujadiliwa Bungeni.

Miss Universe Flaviana Matata akiwa na Mkurugenzi wa Compass communicayion, Maria Sarungi wakiwasha mshumaa kwenye kaburi la Marehemu mama yake mzazi aliyefariki katika ajali ya MV Bukoba mwaka 1996.

Waziri wa mahusiano ya Ulaya na Biashara za kimataifa wa Finland, Alexander Stubb, akifanya mahojiano na Meneja Mahusiano wa Vodacom Tanzania, Bw.Matina Nkurlu katika hafla ya kuingia katika Ushirikiano utakao wawezesha wakulima kupata taarifa za kilimo kupitia simu za mkononi. Pamoja nao ni Waziri wa maendeleo ya kimataifa Heidi Hautala (wa pili kutoka kulia) na Mkurugenzi wa kampuni ya Sibenonke Uwe Schwarz.

Na Lydia Churi.
SERIKALI YAAPA KUWASAKA WAASISI WA VURUGU MTWARA
Serikali imelaani vikali vurugu zilizotokea Mtwara na imeapa kuwasaka waasisi wa vurugu hizo ndani na nje ya Mtwara.
Akitoa kauli ya Serikali Bungeni kuhusu vurugu zilizotokea Mtwara jana, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dkt. Emmanuel Nchimbi ameliambia Bunge kuwa wote waliohusika kupanga, kushawishi, kuandaa na kutekeleza vurugu hizo hawataukwepa mkono wa sheria.
Ndugu zangu,
Mwanafalsafa Jean- Paul Sartre anasema; “ Hell is the other people” – Kwamba jehanam ni wale wengine, anataka pia tukubaliane, kuwa pepo yaweza kuwa ni wale wengine.
Na hakika, tofauti ya mwanadamu na mnyama iko kwenye kufikiri. Mnyama anaongozwa na hisia, lakini mwanadamu anapaswa aongozwe na kufikiri. Ndio maana ng’ombe anaweza kumpanda mama yake. Ni hisia tu zitakazo ongoza tendo lake.

Vurugu hizo zilitokana na hatua ya Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo kusisitiza kuwa bomba la gesi kutoka Mtwara na kuja Dar es Salaam litajengwa, jambo lingine linalodaiwa kusababisha ghasia hizo ni hatua ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kutokurusha moja kwa moja matangazo ya Bunge hivyo kuwakosesha wananchi fursa ya kusikiliza bajeti hiyo.

Na Lydia Churi, MAELEZO-DODOMA
Serikali itaendelea na mpango wake wa kusafirisha gesi asilia kutoka mkoani Mtwara, Lindi hadi Dar es Salaam. Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo ameliambia bunge jana mjini Dodoma alipokuwa akiwasilisha bajeti ya wizara yake ya mwaka wa fedha 2013/2014.

Na Lydia Churi,
Watu milioni mbili hufariki kila mwaka na asilimia nne ya matatizo ya kiafya duniani hutokana na matumizi ya pombe.
Akijibu swali bungeni mjini Dodoma Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Seif Seleman Rashidi alisema Serikali inawataka watanzania kutokutumia pombe kupita kiasi kwa kuwa ina madhara kwa afya zao, familia na taifa kwa ujumla.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisoma hotuba yake ya ufunguzi wa Maonyesho ya Nane ya Vyuo Vikuu kutoka nchi mbalimbali, yatakayofanyika kwa siku tatu katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisikiliza maelezo kutoka kwa, Makamu Mwenyekiti wa Chuo Kikuu cha United African-Tanzania, Jo, Do Hyun, kuhusu matumizi ya gari ndogo inayotumia Chaji ya Umeme wakati alipotembelea katikia Banda hilo,kwenye Maonyesho ya Nane ya Vyuo Vikuu kutoka nchi mbalimbali yanayofanyika kwa siku tatu katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam

Baadhi ya washiriki wa maonyesho ya Nane ya Vyuo Vikuu kutoka nchi mbalimbali, wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, wakati akisoma hotuba yake ya kufungua rasmi maonyesho hayo ya siku tatu katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam. Picha na OMR

JK akiweka jiwe la msingi Barabara ya Iringa –Dodoma .

Rais Jakaya Mrisho kikwete akiongea na wananchi wa Iringa

Baadhi ya wananchi walio hudhulia

JK akipanda mti baada ya kuweka jiwe la msingi
Picha na Said Ng'amilo (mjengwablog)

Katibu Mkuu Maliasili na Utalii Bi. Maimuna Tarishi alianza ziara yake Same kwa kufika ofisini kwa Mkuu wa Wilaya ya Same Mwalimu Herman Kapufi kujitambulisha.
Angalia Picha zaidi...
Ndugu zangu,
MTANZANIA mwenzetu marehemu Shaaban Robert anaandika;
” Wasadikika wana desturi ya kutafuta fimbo baada ya kuumwa na nyoka. Tumekwisha umwa na nyoka kwa matendo yetu mabaya ya zamani.
Nyoka mwenyewe amekwishakimbia. Hapatikani kwa kujilipiza kisasi, lakini, sumu yake imebakia katika jeraha tulilolipata. Sasa, shauri lililo jema ni kuzuia sumu hii isienee miilini mwetu ikaleta kifo.
Maovu yana hatari kubwa kukaa kati yetu. Tumedumu nayo kwa muda mrefu. Hayakutuletea faida ila hasara, huzuni na kilio siku zote.”- Shaaban Bin Robert.
Yanayotokea Mtwara Na Kinachohitajika Sasa...
Ndugu zangu,
Wakati nikisoma na kuangalia kwenye taarifa za habari juu ya vurugu za polisi na vijana kwenye viunga vya Stockholm, na zenye sura ya ubaguzi pia, nimekumbuka juu ya kazi niliyoshiriki kuifanya kitaifa katika nchi ya Sweden mwaka 2003. Ilikuwa ni mwaka mmoja kabla ya kuondoka Sweden kuja kufanya kazi hapa Iringa.
Nikiwa mwanaharakati wa haki za binadamu ikiwamo kupinga vitendo vya kibaguzi niliyeishi Sweden kwa miaka 11, niliteuliwa kuwa mmoja wa watu 12 walioandaa rasimu iliyopelekea kuundwa kwa Kituo cha kwanza dhidi ya ubaguzi katika Sweden. Kituo hicho kilichokuja kujulikana kama ' Center Against Rasicm' kwa Kiswidi ' Centrum Mot Rasism' kilifunguliwa rasmi mwaka 2004 kama inavyooenekana hapo chini kwenye taarifa fupi ya kituo hicho kwa lugha ya Kiswidi.

SHIRIKISHO la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limemteua mwamuzi kutoka Afrika Kusini kuchezesha mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia, Kanda ya Afrika kati ya Tanzania (Taifa Stars) na wenyeji Morocco (Lions of the Atlas).
Mechi hiyo ya kundi C itachezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech, Morocco kwenye Uwanja wa Grand kuanzia saa 3 kamili usiku kwa saa za Morocco. Mwamuzi atakayechezesha mechi hiyo ni Fraser Daniel Bennett.
Bennett atasaidiwa na Thusi Zakhele Siwela pia wa Afrika Kusini, wakati mwamuzi msaidizi namba mbili atakuwa ni Marwa Range kutoka Kenya. Mwamuzi wa akiba (fourth official) ni Lwandile Mfiki wa Afrika Kusini.

Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango akichangia hoja bungeni leo

Habari zilizotufikia muda huu zinaripoti kwamba hali sio nzuri huko Mtwara, kwa ufupi hali ni tete na hakuna amani, mabomu ya machozi yanarindima muda huu na huduma zote za kijamii zimefunngwa hakuna usafiri, masoko, maduka na bar zote zimefungwa, daladala, Taxi na Bodaboda hazifanyi kazi. Kwa ujumla kinachoendelea ni mapambano makali kati ya Jeshi la polisi na wananchi wenye hasira wanaopinga vikali kuendelea kwa mchakato wa gesi ilihali nchi ikiwa haina sera inayosimamia nishati hiyo.
Kwenye shughuli ya kuwekwa jiwe la msingi wa ujenzi wa barabara ya Iringa - Dodoma. Picha zote na Said Ng'amilo wa Mjengwablog.

Pilika pilika za maandalizi.

Uwekaji jiwe la msingi Barabara ya Iringa - Dododma, Hapa na kijiji cha Migori Mkoani Iringa.

Baadhi ya viongozi wakimsubiri mgeni rasmi

Muonekano wa sehemu ya Barabara hiyo.
Picha na said Ng'amilo (mjengwablog)
MAHALI : MAELEZO –IPC
TAREHE : 23/05/2013
MUDA : SAA 5.00 ASB
MKURUGENZI WA HOSPITALI YA IMTU MBEZI BEACH DAR ES SALAAM DR. ALI MZIGE ATAZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI KUHUSU SIKU MAALUM YA KAMBI YA KUPIMA AFYA YA WATOTO WENYE UMRI CHINI YA MIAKA MITANO BILA MALIPO.

Ndugu zangu,
Kumetokea vurugu kati ya polisi na vijana kwenye viunga vya Stockholm, Sweden.
Moja ya tafsiri zake ni tatizo la ubaguzi na kukosa ajira na hususan kwa vijana.
Na kwa vijana wengi wasio na asili ya Sweden wamejisikia kuwekwa kando kwenye jamii, na hivyo kuamsha hasira na hata kutenda mambo ya vurugu ikiwamo kuchoma magari moto na uharibifu mwingine wa mali.
Kuna haja ya vijana kuingizwa kijamii na kitamaduni katika nchi ambayo ama wao wenyewe au wazazi wao walihamia. Ni kazi ngumu, lakini lazima ifanyike.
Maggid,
Iringa.

Enzi za Relwe basi likitoka Dar na kuharibika Mikumi dereva atasubiri mafundi wa Relwe watoke Iringa! Hapo mnaweza kulala hata siku mbili. Pichani ni barabara ya Iringa- Dodoma. Leo Rais Jakaya Kikwete anaweka jiwe la msingi la ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami. Litawekwa pale Migoli, Mtera. Hakika, tumetoka mbali. ( Picha ya Maktaba)

Kwa video za matukio mbalimbali yanoyotokea Tanzania.

HALI YA HATARI, MATUKIO ZAIDI KATIKA PICHA IRINGA LEO.
vurugu iringa mjini
meza ya magazeti leo jumanne
Kipanya Leo
Gesi; Tunagombania bakuli za supu, ng’ombe hajachinjwa!
Unyama mkubwa Mbeya, wawili wazikwa hai
Read more...